JINSI YA KUANDAA CHAKULA CHA KUKU

Somo hili ni  mahususi kwa ajili ya wafugaji wote wa kuku, au kwa wale wote ambao wanapenda kufuga kuku. Kwani mfumo huu ni mzuri na humsaidia mfugaji kuweza kutengeza chakula ambacho kina virubishio vyote ambavyo ni muhimu kwa kuku.

JINSI KUANDAA CHAKULA CHA KUKU KUANZIA WIKI LA 1- HADI WIKI LA 8.
Mahitaji.
1.    Pumba 60kg
2.    Mahind ya kuparaza 10kg
3.    Mashudu alizeti 10kg
4.    Dagaaa 15kg
5.    unga wa mifupa 5kg
6.    Chumvi ½
7.     premix ¼
Mara baada ya kuanda mahitaji hayo changanya vyote ili kupata mchnganyiko wa chakula.

CHAKULA CHA KUKU, KUANZIA WIKI LA NANE NA KUENDELEA.
Mahitaji
1. Pumba ya mahindi yenye chenga- kg 38
2. Mashudu ya alizeti- kg 7.5
3. Mabaki ya dagaa - kg 1.5
4. Chokaa ya kuku - kg 0. 5
5. Unga wa mifupa - kg 0.5
6. Lusina - kg 2
7. Chumvi - kg 0.25
Mara baada ya kuanda mahitaji hayo changanya vyote ili kupata mchnganyiko wa chakula.

2 Comments

  1. Kujua njia bora za ufugaji wa kuku wa kienyeji naomba mni saidie

    ReplyDelete
  2. Premix ni nin na naipataje maana mahitaj hayo mengine ni rahis

    ReplyDelete