UFUGAJI BORA WA KUKU AINA YA KULOIREL

Kuloirel ni kuku chotara ambaye asili yake ni nchini india, na imetokana na mchanganyiko wa  dume la broiler na jike aina ya Rhode island red au dume la white legham na jike la Rhode island red. Kuku hawa ni moja kati ya kuku wasio na gharama kubwa katika kuwafuga lakini pia wana faida kubwa pindi ukiamua kuwafuga. Lakini pia
kuku hawa ni moja kati ya mbegu ambayo inafanya vizuri sana katika nchi nyingi.


SIFA ZA KULOIREL

1.       Ni aina ya kuku ambao hutumika kwa matumizi ya ani nyama pamoja na mayai

2.        Kuku mmoja anauwezo wa kutaga mayai 150 hamsini kwa mwaka ukilinganisha na kuku wengine hutoa 40- 50 kwa mwaka.

3.       Madume ya  kuloirel hua yana kilo 3.5  na jike ni kilo 2.5  ukilinganisha na kuku wengine dume hua na kilo 2.5 na jike ni kilo 1.5.

4.       Pia ni moja kati ya aina ambayo haipati magonjwa kirahisi (disease resistance)


5.       Kuku hawa hawana gharama sana katika kuwalisha kwa sababu wanauwezo pia wa kula chakula kama kuku wa kienyeji. 

              

Banda 
Kama walivyo  kuku wengine banda lazima liwe bora ili kuweza kupata kuku bora pamoja na mayai mengi, ila pia kuku wa aina ya kuroiler sio lazima uwafungie ndani moja kwa moja unaweza kutengeneza sehemu ambayo utawafungulia ili kuweza kujipatia chakulatofauti na kuku wa kisasa.

Lakini pia ni vyema kila wakati ukazingatia usafi ni muhimu hivyo ni vyema kuzingatia hilo 

chakula

Chakula ni lazima kiwe bora ili kupata kuku bora pamoja na mayai ya kutosha.

1.       Kuku jike mmoja anakadiliwa kula kilo 5-8 kabla ya kuanza kutaga.

2.       muhimu sana kwa mfugaji kujifunza jinsi ya kuchanganya chakula mwenyewe.


3.       kuanzia siku 1 hadi wiki 4 unatakiwa kuwapa chakula cha kuanzia (chick starter mash)

4.       kuanzia wiki ya 4 hadi 8 unawapa chakula cha kukuzia (chick grower mash)


5.       Kuanzia wiki ya kwanza kuanza kutaga hadi mwisho unatakiwa kuwapa chakula(layersmash)
6.        
7.       Lakini pia inakadiliwa kua na drinker 15 na vyombo vya kulia chakula, wastani wa kuku 1000.

7 Comments

  1. Kuku aina ya kroiler ni mkombozi wa mgugaji!!!!

    ReplyDelete
  2. Kuku hawa waweza kuwafuga kwenye cages za kutengeneza mwenyewe?

    ReplyDelete
  3. Nafuga hao kuku .wameanza kutaga vizuri tu lakini kwa sasa wanataga mayai ambayo bado hajayakomaa tatizo nini .

    ReplyDelete
  4. Nikiitaji kuwa funga bitawapataje?mimi naishi Rukwa

    ReplyDelete
  5. Kuku aina hii wanapatikana mikoa gani haswa

    ReplyDelete
  6. Ningependa kujua nawezaje kupata mbegu ya kloila na vifaranga ni kiasi gani

    ReplyDelete